Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Idadi ya maambukizi ya COVID-19 yapungua, nchi yarekodi visa 137, 18 waaga dunia

0d49d16e80a04ecf Idadi ya maambukizi ya COVID-19 yapungua, nchi yarekodi visa 137, 18 waaga dunia

Mon, 3 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Waziri Kagwe ametangaza kwamba watu wengine 137 wamethibitishwa kuwa na virusi vya COVID-19

- Wengine 18 wamepoteza maisha yao hii leo, Jumatatu, Mei 3 na kupelekea jumla ya vifo nchini kufikia 2, 781

- Kufikia sasa nchi imerekodi sampo 160, 559 zilizofanyiwa vipimo na visa 1,681,420 vya maambukizi kwa jumla

Wizara ya Afya imetangaza kwamba watu wengine 137 wamepatikana na virusi vya COVID-19 kutokana na sampo 1,641 zilizofanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Kulingana na hotuba ya Waziri Mutahi Kagwe aliyoitoa kwa umma Jumatatu, Aprili 3, msambao wa maambukizi kote nchini uko kwenye asilimia 8.3%.

Kati ya visa vilivyoripotiwa, 129 ni Wakenya, 8 ni raia wa nchini za kigeni; kijinsia 80 ni wanaume na 57 ni wanawake.

Mgonjwa mdogo ana umri wa miaka 14 ilhali mkubwa ana umri wa miaka 97.

Kufikia sasa nchi imerekodi sampo 160, 559 zilizofanyiwa vipimo na visa 1,681,420 vya maambukizi kwa jumla.

Watu wengine 18 wamepoteza maisha yao chini ya saa 24 zilizopita na kupelekea idadi jumla ya vifo kufikia 2, 781 kulingana na takwimu za wizara ya afya.

Aidha, watu 1, 265 wamelazwa katika hospitali mbali mbali nchini, 6,614 wakiwa chini ya ulinzi wa kimatibabu wa nyumbani.

Wagonjwa 179 wamelazwa katika vyumba vya ICU, 29 kati yao wakiwa kwenye ventileta na 110 wakiwa wamewekwa kwenye oksijeni.

Waziri Kagwe pia alitangaza kuwa kufikia Mei 3, watu 887, 034 kwa jumla walikuwa wamepokea chanjo ya virusi vya corona kote nchini.

Haya yanajiri siku mbili baada ya Rais Uhuru Kenyatta kufungua mipaka ya kaunti tano ikiwemo Nairobi, Nakuru, Kiambu,Kajiado na Machakos ambayo ilikuwa imefungwa Machi 26 kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya COVID-19.

Rais pia aliongeza saa za kafyu kutoka saa mbili hadi saa nne usiku na kukamilika saa kumi alfariki.

Akihutubia taifa akiwa Ikulu ya Nairobi siku ya Leba Dei, Jumamosi Mosi, Uhuru pia alitangaza kuwa mahoteli na baa zifunguliwe ila kufikia saa moja jioni ziwe zimefungwa.

Vile vile Uhuru alisema tarehe ya kufungua shule inasalia kuwa 10 Mei kama ilivyoratibiwa na wizara ya Afya.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke