Thu, 14 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Idadi ya vifo vilivyotokana na mafuriko ambayo yameharibu eneo la pwani karibu na mji wa bandari wa Durban nchini Afrika Kusini imeongezeka hadi zaidi ya 250, maafisa wanasema.
Hapo awali ilikadiriwa kuwa takriban watu 59 walikuwa wamefariki katika jimbo la KwaZulu-Natal.
Nomagugu Simelane, waziri wa afya wa KwaZulu-Natal, aliambia shirika la utangazaji la eNCA la Afrika Kusini kuwa watu 253 wamefariki.
Shirika la habari la Reuters linasema maafisa wa mkoa sasa wameweka idadi hiyo kuwa 259.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live