Jeshi la Kenya limethibitisha kwamba ibada ya wafu kuwakumbuka wanajeshi wote itafanyika Jumamosi Aprili 20 kwa heshima na muongozo wa kidini itakayoongozwa na viongozi wa kidini ambao pia ni wanajeshi.
Uchunguzi umeidhinishwa kubaini chanzo cha ajali ya ndege katika kaunti ya Elgeyo Marakwet iliyosababisha vifo vya maafisa 10 wa kijeshi akiwemo mkuu wa majeshi ya Kenya Jenerali Francis Ogola.
Haya ni wakati maandalizi ya mazishi ya Jenerali Ogola yakiendelea, akiatarajiwa kuzikwa siku ya Jumapili huku maafisa wengine wawili waliofariki katika ajali hiyo wakizikwa siku ya Ijumaa
Rais William Ruto ameongoza ujumbe kutoka serikalini kuifariji familia ya jenerali Ogola.
Ibada fupi iliandaliwa nyumbani kwa Jenerali aliyefariki huku Amiri jeshi Mkuu wa majeshi ya Kenya akitoa taarifa yake kwa familia ambayo imetoa muelekeo wa marehemu kuhusu mazishi yake.