Shirika la Fedha Duniani (IMF) limeipa Sudan Kusini mkopo wa dola za Marekani Milioni 334 kwaajili ya kusaidia shughuli za kiuchumi nchini humo, taarifa ya Benki Kuu ya Sudan imeeleza.
Mapema mwezi March 2021, Shirika la Fedha (IMF) liliipa Sudan Kusini kiasi kingine cha mkopo wa Dola za Marekani Milioni 172.2 kwaajili ya kuinua uchumi wan chi hiyo ambayo imekua ikipitia vipindi vigumu baada ya kumalizika kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Baada ya kupokea fedha hizo, Benki Kuu ya Sudan mwezi April 2020 huu ilitangaza kuanza kuingiza fedha za kigeni kwenye mabenki ya nchi hiyo ili kuongeza kasi ya ukuaji uchumi. Mpaka kufikia December 2020 imeshaingiza dola milioni 30 kwenye mzunguko wa fedha nchini humo.