Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huzuni, mke akihudhuria mazishi ya mumewe akiwa kwenye machela

Df93b537a80c657c Huzuni, mke akihudhuria mazishi ya mumewe akiwa kwenye machela Bomet

Wed, 17 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kulikuwa na wimbi la simanzi Bomet baada ya mwanamke mgonjwa kuwasili katika mazishi ya mume wake Jumatatu, Novemba 15, na ambulensi akiwa amelala kwenye kitanda cha wagonjwa.

Mnamo Novemba 2, 2021, familia moja Bomet ilipata pigo kubwa baada ya wazazi wao kuhusika katika ajali baba yao alifariki papo hapo. Mama yao aliachwa na majeraha mabaya na kulazwa katika Hospitali ya Longisa ambapo amekuwa akipokea matibabu.

Waombolezaji walighubikwa na simanzi baada ya mwanamke huyo kuwasili katika mazishi ya mume wake na ambulensi akisalia kwenye kitanda cha wagonjwa hafla nzima.

Joseph Rotich, mume wake Regina Rotich, aliangamia katika ajali mbaya ya barabarani mnamo Novemba 2, 2021, na mwanamke huyo aliponea tu chupuchupuna kupata majeraha mabaya na kushudiwa kuwasili katika mazishi ya mume wake akisalia kwenye kitanda cha wagonjwa.

Akizungumza na TUKO.co.ke, mtoto wa tatu wa wanandoa hao Nick Kimutai alisimulia tukio hilo la kutisha ambapo wazazi wake walikuwa kwenye pikipiki siku hiyo ya mauti ambayo baba yake alipoteza maish

"Baba yangu alifariki papo hapo baada ya kuvunjika kichwa huku mguu wake wa kulia ukivunjika na kwa hakika ulikuwa umetenganishwa na mwili," alisimulia maelezo ya kusikitisha ya ajali iliyotokea wakati wanandoa hao walipogongana na roli lililokuwa barabarani.

Mama yake Kimutai alilazwa katika Hospitali ya Longisa baada ya kupata majeraa kwenye mguu wake wa kulia na nyonga.

Majeraha yake yalikuwa mabaya zaidi na kumfanya kushindwa kusimama wakati wa mazishi ya mume wake Joseph Rotich ambapo pamoja wameweza kujaliwa tato sita.

Katika picha za huzuni zilizopakiwa na Kimutai, Regina alisalia kwenye kitanda cha wagonjwa hafla nzima.

Huku watoto wa Rotich wakiwa na wasiwasi ya namna wataweza kulipa bili ya hospitali ya mama yao inayoendelea kuongezeka, anatakiwa kufanyiwa uchunguzi zaidi ya kimatibabu kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.

Wiki jana, Kimutai alisema familia hiyo ilitumia KSh 80,000 kwa matumizi ya nje pekee na pia anahofia karo ya wadogo wake ambao bado wako katia shule za sekondari.

"Hapo zamani tulikuwa familia yenye furaha lakini nyumbani kwa sasa kumeachwa bila watu. Mama amelazwa hospitalini na bili kubwa inatusubiri. Ombi langu ni tushikane mikono kuokoa maisha ya mama. Unaweza kutusaidia kwa kutuma kiasi chochote kwa +254701734411," alisema.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke