Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huzuni Jenerali Katumba akiondoka hospitalini kwenda kutizama mwili wa bintiye

F03e49dd8f8a195a Huzuni Jenerali Katumba akiondoka hospitalini kwenda kutizama mwili wa bintiye

Thu, 3 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Aliyekuwa mkuu wa majeshi nchini Uganda Jenerali Katumba Wamala aliruhusiwa kuondoka hospitalini Jumanne, Juni 2

- Mwanajeshi huyo aliungana na wamombolezaji kuutizama mwili wa bintiye Brenda Katumba nyumbani kwake Najeera

- Katumba alinusurika kifo baada ya gari lake kumiminiwa risasi, bintiye alifariki dunia kwenye shambulizi hilo

Aliyekuwa mkuu wa majeshi nchini Uganda Katumba Wamala ameruhusiwa kuondoka hospitali baada ya kupokea matibabu kutokana na majeraha ya risasi.

Katumba alifululiza hadi nyumbani kwake kuutizama mwili wa bintiye mwenye umri wa miaka 32 ambaye aliuawa na watu wasiojulikana.

Brenda alipoteza maisha yake akiwa ameandamana na babake ambapo gari lao lilimiminiwa risasi, Katumba alinusurika kifo kwenye shambulizi hilo.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.coke, Katumba alimshukuru Mungu kwa kumuepusha na kifo ingawa alimpoteza bintiye brenda.

Afisa huyo mkuu pia alimshukuru Rais Museveni, wahudumu wa afya wabunge na mhudumu wa boda boda aliyekimbikiza hospitalini baada ya kupigwa risasi.

" Ningependa kumshukuru Rais Yoweri Museveni kwa kunijali kiwango hiki, simu alizokuwa akinipigia kunijulia hali ndizo zinafanya kwa sasa bado napigania maisha yangu, pia ningependa kumshukuru mhudumu wa boda boda ambaye alinilazimisha kunibeba kwenye piki piki yake na akahakikisha amenifikisha hospitali kwa huduma ya kwanza,

" Ningependa pia kushukuru wahudumu wa afya katika hospitali ya Malcolm Healthcare Kisasi kwa kila juhudu waliofanya kuhakikisha napata huduma inayostahili," Wamala alisema.

Iliripotiwa kuwa watu wawili wasiojulikana wakiwa wamejihami kwa bunduki, walimiminia gari la mawanajeshi huyo na risasi kadhaa siku ya Jumanne, Juni 1 katika barabara ya Kisota eneo la Kisaasi.

Wamala alikuwa ndani ya gari lake na bintiye mbaye alipoteza maisha yake kwenye shambulizi hilo, uchunguzi umeanzisha kubaini chanzo na waliohusika kwenye shambulizi hilo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke