Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hustler Tosha: Aliyekuwa naibu gavana Jonathan Mueke ajiunga na DP Ruto

56da8200565d1e71 Hustler Tosha: Aliyekuwa naibu gavana Jonathan Mueke ajiunga na DP Ruto

Fri, 30 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mueke anamezea kiti cha ugavana cha Kitui na sasa duru zinaarifu atawania nafasi hiyo kwa tiketi ya UDAChama cha UDA kinahusishwa na Nabu Rais William Ruto na kimeanza kupenya katika ngome za vigogo wengine DP amekuwa akitafuta makamanda ambao watamsaidia kupenya ngome hizo akijiandaa kwa kampeni za 2022Aliyekuwa Naibu Gavana wa Nairobi Jonathan Mueke Ijumaa Julai 30 alikutana na Naibu Rais William Ruto.

Mueke alisema amevutoiwa na injili ya DP kuhusu mfumo mpya wa kiuchumi nchini ambao anasema utabadili maisha ya Wakenya.

"Nimekutana na DP na kuskiza kwa karibu jinsi mfumo wake wa kiuchumi wa bottom up utawainua Wakenya wengi, nimevutiwa na kuamua kujihusisha na sera zake," alisema Mueke baada ya kikao chake na DP Karen.

Meza ya TUKO.co.ke imepata ripoti kuwa mwanasiasa huyo anamezea mate kiti cha ugavana kaunti ya Kitui katika uchaguzi wa 2022.

Mueke amekuwa ni kiungo muhimu katika chama cha Wiper katika siasa za 2013 na 2017 ambapo aliteuliwa kama mgombea mwenza wa Evans Kidero 2013.



Read also

"Uchumi Ndio Form": Ujumbe wa DP Ruto kwa Wapinzani Wake

Wawili hao walishinda uchaguzi huo kwa tiketi ya ODM na kuhudumu hadi 2017 wakati timu ya Mike Sonko na Polycarp Igathe ilichukua mamlaka.

Viongozi kadhaa humu nchini wamekuwa wakiingia kambi ya Ruto kipindi hiki ambapo anajipanga kuwania urais 2022.



DP amekuwa akitafuta makamanda ambao watamsaidia kupenya ngome za Rais Uhuru Kenyatta, Raila Odinga na Kalonzo Musyoka.

Tayari amewashika wabunge kadhaa kutoka Ukambani na pia bwanyenye wa eneo hilo Johnstone Muthama.

Vile vile, DP yuko na kundi la viongozi katika eneo la Mlima na Pwani ambapo kufikia sasa amepata umaarufu.

Kuingia kwa Mueke ndani ya hustler Nation kutawezesha DP kujaribu kupenya kaunti ya Kitui ambapo Charity Ngilu ndiye gavana.

Ngilu ni mmoja wa wakosoaji wakuu wa DP na amekuwa akiwarais Kalonzo na Raila kuungana ili waweze kumshinda Ruto.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke



Read also

Hisia Mseto Baada ya Kalonzo Musyoka Kukutana na Muthama
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke