Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Human Rights yawashutumu wanajeshi wa Rapid Support Forces

Human Rights Yawashutumu Wanajeshi Wa Rapid Support Forces Human Rights yawashutumu wanajeshi wa Rapid Support Forces

Thu, 9 May 2024 Chanzo: Bbc

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch linasema wanajeshi wa Rapid Support Forces wa Sudan na washirika wake wa Kiarabu huenda walifanya mauaji ya halaiki katika mji wa Darfur Magharibi wa El Geneina.

Pia linawatambua makamanda watatu wa RSF waliohusika na ukatili huo, akiwemo kiongozi wa kundi hilo, Mohammed Hamdan Dagalo, maarufu kwa jina la Hemedti.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RSF na jeshi vimezua mzozo mkubwa wa kibinadamu na uhamishaji makazi inapoingia mwaka wake wa pili.

Mengi yameripotiwa kuhusu mawimbi ya mashambulizi dhidi ya wakazi wa El Geneina ambao wengi wao si Waarabu mwaka jana.

Lakini hii ni moja ya uchunguzi wa kina zaidi hadi sasa.

Inahitimisha kuwa RSF na washirika wake wa Kiarabu walifanya uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita kwa kuwalenga Massalit.

Na inazua uwezekano kwamba wanaweza kuwa na nia ya kuharibu jamii ya Darfur Magharibi, ambayo ingeashiria mauaji ya halaiki.

Kiongozi wa RSF Jenerali Hemedti amekanusha wapiganaji wake kuwashambulia raia kimakusudi.

Lakini Human Rights Watch inasema yeye ni miongoni mwa wale walio na jukumu la amri juu ya vikosi vilivyofanya ukatili huo.

Marekani na mwendesha mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wamezungumza kuhusu uhalifu wa kivita kwa pande zote mbili, lakini hawajataja hasa mauaji ya halaiki.

Chanzo: Bbc