Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Human Rights Watch yaishutumu Rwanda kwa kuwaua wakosoaji

Human Rights Watch Yaishutumu Rwanda Kwa Kuwaua Wakosoaji Human Rights Watch yaishutumu Rwanda kwa kuwaua wakosoaji

Tue, 10 Oct 2023 Chanzo: Bbc

Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeishutumu Rwanda kwa kutumia mbinu za ukandamizaji kuwalenga wakosoaji wake nje ya nchi, wakiwemo wale ambao wametafuta ulinzi wa kimataifa.

"Mchanganyiko wa unyanyasaji wa kimwili, ikiwa ni pamoja na mauaji na kupotea kwa watu kutekelezwa, ufuatiliaji, matumizi mabaya ya sheria - za ndani na za kimataifa - unyanyasaji dhidi ya jamaa nchini Rwanda ... ni juhudi za wazi za kuwatenga wakosoaji wanaoweza kuwakosoa," inasema.

Ripoti hiyo imechapishwa wakati Mahakama ya Juu ya Uingereza ikisikiliza rufaa ya serikali ya Uingereza dhidi ya uamuzi unaozuia mipango yake ya kuwafukuza wanaoomba hifadhi nchini Rwanda.

Uingereza haipaswi kuchukulia Rwanda kama nchi salama, ilisema. "[Matokeo] yanabainisha kuwa Rwanda si nchi ambayo Uingereza inapaswa kutegemea kushikilia viwango vya kimataifa au utawala wa sheria linapokuja suala la wanaotafuta hifadhi," alisema Yasmine Ahmed, mkurugenzi wa HRW wa Uingereza.

Rwanda inakanusha madai hayo, huku msemaji wa serikali Yolande Makolo akishutumu HRW kwa "kupotosha ukweli" na "kuendeleza ajenda ya kisiasa".

Katika ripoti yake, HRW ilisema kuwa iliwahoji takriban watu 150 kote duniani katika kipindi cha tangu ushindi wa Rais Paul Kagame mnamo 2017.

Ilisema imeandika dhuluma dhidi ya Wanyarwanda wanaoishi Australia, Ubelgiji, Canada, Ufaransa, Kenya, Msumbiji, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, Uingereza na Marekani, pamoja na jamaa zao nchini Rwanda.

Chanzo: Bbc