Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hukumu kwa waliovamia maduka ya Westgate kutolewa leo

1 1 660x400 Hukumu kwa waliovamia maduka ya Westgate kutolewa leo

Tue, 6 Oct 2020 Chanzo: millardayo.com

Hukumu ya washukiwa wa mlipuko wa kigaidi katika jengo kubwa la maduka la Westgate jijini Nairobi mwaka 2013 na kusababisha vifo vya watu 67 inatarajiwa kutolewa leo Jumanne baada ya kuahirishwa jana.

Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo amesema kuna mambo yalikuwa hajakamilika, na hivyo kulazimika kuahirisha uamuzi huo kwa mara nyingine.

Watu 67 waliuawa katika shambulio hilo ambalo wanamgambo wa kundi la al-Shabab walidai kulitekeleza.

Kundi la Al-Shabab linaendelea kuwa tishio kwa usalama wa kanda hii kutokana na jinsi limekuwa likibadilisha mbinu ya mashambulizi katika taifa jirani la Somalia ambalo ndio chimbuko lao.

TAZAMA BALOZI AVUA BARAKOA MBELE RAIS MAGUFULI, AMPONGEZA JPM IKULU

Chanzo: millardayo.com