Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hotuba ya Raila yakatizwa na vijana waliokuwa wakiimba sifa za DP Ruto

03004356c7c48036 Hotuba ya Raila yakatizwa na vijana waliokuwa wakiimba sifa za DP Ruto

Tue, 19 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Hotuba ya Raila Odinga kwa wakaazi wa Meru ilisambaratika baada ya vijana kuanza kuimba nyimbo za kumsifia Naibu Rais William Ruto.

Katika kila sentensi aliyotamka, wenyeji walijibu "Ruto!" Katika mkutano uo huo, kinara huyo wa Upinzani alisema mchakato wa BBI ambao ulifutiliwa mbali na mahakama ulikuwa mapumzikoniSafari ya Kinara wa Orange Democratic Movement (ODM) leader Raila Odinga kuukwea Mlima Kenya huenda imeanza kukumbwa na misukosuko baada ya wenyeji wa Meru kumsifia Ruto akiwahutubia.

Waziri Mkuu huyo wa zamani ambaye yuko katika harakati ya kuwashawishi zaidi ya wenyeji milioni tano wa Mlima Kenya kumuunga mkono amekuwa akizunguka kote chini katika miezi ya hivi punde.

Hata hivyo, ziara yake manmo Jumanne, Oktoba 19 ilitatizika huko Meru baada ya baadhi ya umati uliokuwa umekusanyika kumsikiza kuanza kumzomea wakiimba nyimbo za kumsifu Naibu Rais William Ruto.

Katika kila sentensi ambayo Raila alisema, wenyeji wa Meru walipiga kelele wakisema "Ruto!" kuvuruga hotuba yake ambayo alikuwa akiwasilisha sera zake katika kivumbi cha kuwania urais 2022.

"Umoja ,!" alisema huku nao wakazi wakisema "Ruto".

Raila:

"Uchumi bora!" Tena, kwa sauti ya juu wenyeji waliimba kwa pamoja "Ruto"

Raila:

"Vijana tibim?" nao wakajibu "Ruto".

Katika mkutano uo huo, mgombea huyo wa urais mara nne pia alisema mchakato wa BBI ambao ulifutiliwa mbali na mahakama ulikuwa mapumzikoni huku wenyeji hao wakizidi kuimba.

Haya yanajiri siku moja baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuwauliza "wanajeshi" wake katika Mlima Kenya kuwa makini mno kuwahusu wanasiasa ambao wanataka kuwatapeli kura zao.

Katika kile kilichoonekana kama shambulizi la moja kwa moja kwa naibu wake William Ruto, rais aliwahimiza wenyeji kumsikiza kila mmoja anayewania urais na sera zake kabla ya kufanya maamuzi ya busara.

Kiongozi wa nchi alishikilia kwamba wakati wa kampeni bado haujawadia ila wakati mwafaka utakapofika atawapa mwelekeo ambao watauchukua.

"Nyinyi watu mnadanganywa sana. Mbona msiwaambie kile mnachotaka ni uwezeshaji? Watu wangu jamani amkeni na mfahamu mambo ambayo yatawafaidi nyinyi na vizazi vyenu," alisema huku umati ukisahngilia.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke