Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Homa ya dengue yaua mmoja na wengine 41 wakiugua

Homa Ya Dengue Homa ya dengue yaua mmoja na wengine 41 wakiugua

Thu, 19 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Chad imethibitisha kifo kimoja kutokana na mlipuko wa homa ya dengue na zaidi ya kesi 1,342 zilizoshukiwa kufikia sasa, ikiwa ni pamoja na 41 ambazo zimethibitishwa.Homa

Takwimu hizi ni hadi mwanzoni mwa Oktoba zinazofunika kipindi tangu nchi hiyo ilipotangaza mlipuko wa dengue mwezi Agosti, kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Wizara ya afya ya Chad kwa sasa inakabiliana na mlipuko huo huku kukiwa na wasiwasi wa ugonjwa huo kusambaa zaidi kwa sababu ya uwezo mdogo wa ufuatiliaji na usaidizi.

Wilaya ya afya ya Abéché, katika mkoa wa kusini mashariki wa Ouaddai, ndio kitovu cha mlipuko wa sasa.

Dengue huambukizwa na mbu na mara nyingi husababisha dalili kali kama za mafua, bila matibabu maalum. Utambuzi na usimamizi wa wakati ni muhimu.

Kesi katika jamii zinaweza kuripotiwa kwa sababu waganga mara nyingi huchanganya dalili zake na maambukizi mengine, na kufanya utambuzi wa mapema kuwa changamoto, haswa katika maeneo yenye vifaa vichache vya upimaji.

WHO inataja mlipuko huo kama hatari kubwa ya kitaifa kutokana na mazingira mazuri ya kuenea kwa mbu na mgogoro unaoendelea wa kibinadamu katika eneo linalohusisha utitiri wa wakimbizi kutoka Sudan.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live