Wed, 16 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Bunge la Kitaifa limethibitisha kupokea mapingamizi 4 ya kuwafuta kazi Maafisa 4 wa Tume Huru ya Uchaguzi waliodai Matokeo ya Urais hayakuwa halali.
Makamu Mwenyekiti wa Tume, Juliana Cherera, na Makamishna Francis Wanderi, Justus Nyang’aya na Irene Masit walipinga matokeo yaliyotangazwa na Mwenyekiti Wafula Chebukati.
Maafisa hao watajua hatma yao ndani ya siku 14 baada ya Kamati ya Bunge kuwasilisha ripoti ambayo Bunge litamtaka Rais Ruto kuunda Tume ya Majaji itakayochunguza kama wanapaswa kubaki au kuondolewa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live