Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hisia Mseto Baada ya Mbunge Ndindi Nyoro Kukiuka Agizo la Rais

F08e0978aa070ede Hisia Mseto Baada ya Mbunge Ndindi Nyoro Kukiuka Agizo la Rais

Sat, 27 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Nyoro alihudhuria mkutano wa harambee uliokuwa ukichangisha fedha za kuinua mradi wa maji katika eneo bunge lake

- Wakenya walihisi mbunge huyo alikuwa akiwaweka wakazi kwenye hatari ya kuambukizwa maradhi ya Covid-19

- Wengine walimkosoa Nyoro kwa kukosa kuheshimu amri iliyotolewa na Rais Uhuru Kenyatta Ijumaa Machi 26

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro amezua hisia mseto kwenye mtandao baada ya kuhudhuria kongamano licha ya Rais Uhuru Kenyatta kupiga marufuku mikutano yote.

Kwenye hotuba yake Ijumaa Machi 26, Rais Uhuru alisema mikutano ya aina yote imepigwa marufuku katika juhudi za kupigana na maambukizi ya coronavirus.

Mbunge huyo wa kambi ya kisiasa ya Tangatanga alikuwa katika eneo la kibiashara la Mitundu ambapo walifanya harambee.

"Mradi huu chini ya Upper Tana utagharimu milioni 5.5. Jamii inachangisha asilimia kumi ambayo inahitajika na tumejitahidi vilivyo. Asante sana kwa uongozi wa kundi hili Amos Kiiru, Kamau, na Kaguongo," Nyoro alisema.

Wakenya walikerwa na mbunge huyo kutokana na mkutano huo wakisema ni tishio kwa wakazi kutokana na janga la coronavirus.

"Kwa hivyo ni kweli kuwa sheria huwekwa ili zivunjwe? Kwa kweli unawajali wakazi ukijua vizuri kuwa hawawezi kupata KSh 650, 000 ambazo zinahitajika kulazwa ICU?" alisema Martin Mburu

"Unahatarisha maisha ya watu. Si vizuri ukijua wewe uko na uwezo wa kugharamia bili za hospitali tofauti na wakazi hao," alisema Nzuva.

"Hii inaudhi sana . . . unakosa heshima kwa binadamu ...fanyeni michango kupitia mitandao," Priscilla Waithira alisema.

Wizara ya Afya imekuwa ikiwaonya Wakenya kuhusu wimbi la tatu la maradhi ya Covid-19 ambalo wanasema lilianza mwezi Machi.

Wataalamu wamesema huenda makali ya maradhi hayo yakawa moto hadi kufia mwezi Mei.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke