Wed, 29 May 2024
Chanzo: Bbc
Rais Cyril Ramaphosa amepiga kura yake katika kituo cha Chiawelo huko Soweto, akiandamana na mkewe Tshepo Motsepe.
Anasema ana imani kuwa IEC itasimamia uchaguzi vizuri kwa sababu wao ni wa kiwango cha kimataifa na wamejipanga vyema.
"Hii ni siku kuu kwa demokrasia nchini Afrika Kusini. Leo tunapigia kura utulivu na upanuzi wa demokrasia yetu," aliongeza.
Ana matumaini ya kupata mamlaka mapya ya kuendelea kuongoza nchi.
Chanzo: Bbc