Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hekalu lililopotea Misri kwa miaka 4500 lapatikana

Sun Temple Of Niuserre 8 Hekalu lililopotea Misri kwa miaka 4500 lapatikana

Mon, 15 Nov 2021 Chanzo: BBC

Wanaakiolojia nchini Misri wanasema wamepata moja ya uvumbuzi muhimu zaidi katika miongo kadhaa.

Wamepata mojawapo ya mahekalu manne ya jua yaliyopotea na yaliyojengwa na mafarao wakiwa bado hai katika jaribio la kujigeuza kuwa miungu hai.

Inaaminika kwamba mahekalu sita tu ya jua yalijengwa na mafarao wa Misri miaka 4,500 hivi iliyopita.

Ni mbili tu kati ya hizo sita zimegunduliwa hadi sasa, kwa hivyo wanaakiolojia wanaelezea ugunduzi wa muundo wa tatu kama huo kuwa uvumbuzi mkubwa zaidi ndani ya miaka 50.

Lilikuwa katika eneo la Abu Gorab kusini mwa Cairo na lingekuwa na ukubwa mbao umelingana kikamilifu na upinde wa mashariki-magharibi wa jua.

Ingawa piramidi kubwa ziliundwa ili kuhakikisha hadhi ya farao kama mungu katika maisha ya baada ya kifo, mahekalu ya jua yalikuwa miundo midogo na ilikusudiwa kuwaweka kama miungu hai.

Chanzo: BBC