Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Hatimaye uchunguzi wa maiti kwa mwili wa konstebo Caroline Kangogo wafanywa

CRIME SCENE.png Hatimaye uchunguzi wa maiti kwa mwili wa konstebo Caroline Kangogo wafanywa

Wed, 28 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Uchunguzi wa maiti umeonyesha kwamba Caroline Kangogo alijiuwa kwa kujipiga risasi kwenye kichwaMwanapalojia wa serikali Johansen Oduor alisema risasi iliharibu ubongo wake na kusababisha kuvuja damu nyingiMwendazake afisa huyo Caroline anatarajiwa kuzikwa Alhamisi, Julai 29 nyumbani kwa babake kulingana na taarifa kutoka kwa familiaUchunguzi wa maiti umeonyesha kwamba konstebo Caroline Kangogo alifariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi baada ya kujipiga risasi moja kichwani.

Mwanapalojia wa serikali Johansen Oduor alifanyia upasuaji huo katika hospitali ya rufaa ya Moi Eldoret siku ya Jumanne, Julai 27.

Odour alisema risasi iliharibu fuvu na ubongo wa marehemu na hangeweza kupona hata kama angenusurika kifo.

" Kisa hicho kilitokea katika eneo la tukio, mwendazake alijiua kwa kujipiga risasi moja kwenye kichwa, fuvu na ubongo viliharibika sana," Oduor alisema.



Read also

Siasa Mbaya: Jamaa Adungwa Kisu Mazishini na Kufariki Dunia

Oduor pia alifutilia mbali madai kwamba afisa huyo aliuawa kwingine na mwili wake kuvuta hadi kwenye bafu ya wazazi wake kijijini Anin kaunti ya Elgeyo Marakwet siku ya Ijumaa, Julai 16.

Maafisa wa DCI walisema kuna poda iliyopatikana kwenye mkono wake na itafanyiwa uchunguzi zaidi pamoja na bunduki aliokuwa akitumia afisa huyo.

Mwendazake afisa huyo Caroline anatarajiwa kuzikwa Alhamisi, Julai 29 nyumbani kwa babake kulingana na taarifa kutoka kwa familia.

Uchunguzi wa maiti ulikuwa ufanyika Ijumaa, Julai 23 lakini ulihairishwa kwa sababu Mwanapalojia Oduor hakuwa anapatikana siku hiyo.

Babake Caroline alilia baada ya kunyimwa mwili akidai kwamba angeambiwa mapema kwa sababu mipango ya mazishi ilikuwa imekamilika na alitaka kumzika bintiye Jumamosi, Julai 24.

" Nataka kumzika binti wangu, sina tatizo lolote na yeyote, ninachotaka ni kuchukua mwili wa binti wangu niende niuzike," Alisema babake marehemu.



Read also

Aliyekuwa Mbunge wa Imenti ya Kati Gideon Mwiti Amefariki Dunia

Ingawa Caroline alitaka mwili wake uchomwe, babake alisisitiza kwamba atazikwa kulingana na itikadi za kikiristo.

Kangongo anadaiwa kuwauwa wanaume wawili mmoja akiwa konstebo mwenzake wa polisi na mwingine mfanyabiashara mkubwa, wote wanasemekana kuwa wapenzi wake.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke