Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Guinea: Kanali Doumbouya akataa kukutana na mpatanishi wa ECOWAS

Dombo.png Guinea: Kanali Doumbouya akataa kukutana na mpatanishi wa ECOWAS

Thu, 11 Nov 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkutano wa mwisho wa wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) kuhusu migogoro ya Guinea na Mali, ambao ulifanyika mwishoni mwa juma lililopita mjini Accra, ulimtaja mjumbe maalum wa Tume hiyo nchini Guinea.

Mohamed Ibn Chambas, mwanadiplomasia wa Ghana, ameteuliwa kuwa mpatanishi kati ya jumuiya hiyo ya kikanda na Guinea, iliyowekewa vikwazo na ECOWAS kwa kuchukuwa madaraka kwa nguvu. Lakini mamlaka nchini Guinea inabaini kwamba hakuna mgogoro wa ndani na kwamba mchakato wa mpito uko kwenye njia sahihi. Hii ndiyo sababu Kanali Mamadi Doumbouya, kiongozi mkuu wa mapinduzi huko Conakry, alimwandikia mkuu wa nchi wa Ghana, rais wa sasa wa ECOWAS.

Katika barua hii, rais wa mpito na Mkuu wa Nchi ya Guinea ameandika: "Nimepokea hatua ya viongozi wa kikanda kutambua hatua iliyopigwa katika mchakato wa mpito nchini Guinea. Ameongeza: “Napenda kusisitiza dhamira yangu ya kufanya kila liwezekanalo ili kuendeleza mchakato huu kwa umoja na kwa pamoja, kwa kuzingatia masharti ya katiba ya mpito ambayo ndiyo Katiba ya muda. "

Kanali Doumbouya anasisitiza "utayari wa serikali ya Guinea kudumisha mazungumzo ya mara kwa mara na ushirikiano wa karibu na ECOWAS wakati wa akipindi hiki cha mpito".

Hata hivyo, ameandika, "uteuzi wa mjumbe maalum hauonekani kwetu kuwa wa mwafaka au wa dharura kwani hakuna mgogoro wowote ambao umeonekana ambao unaweza kuhatarisha mwenendo wa kawaida kipindi cha mpito".

Chanzo: www.tanzaniaweb.live