Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gladys Wanga: Chaguzi ndogo zimeonyesha wazi DP Ruto hana wafuasi inavyodhaniwa

557222f9770d0202 Gladys Wanga: Chaguzi ndogo zimeonyesha wazi DP Ruto hana wafuasi inavyodhaniwa

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wanga alidai Ruto amekuwa akisafirisha watu kuhudhuria mikutano yake ili kujenga hisia za uwongo kuhusu umaarufu wake

- Alidai matokeo mabaya ya UDA katika chaguzi ndogo ni dalili wazi ya kitakachotokea mnamo 2022

- Chama hicho kipya, ambacho nembo yake ni Wilbaro, hadi sasa kimeshiriki katika chaguzi ndogo saba na kushinda kiti kimoja tu

Mwakilishi wa Kike wa Kaunti ya Homa Bay Gladys Wanga amesema idadi kubwa ya watu katika mikutano ya Naibu Rais William Ruto haimaanishi atapokea kura nyingi 2022.

Habari Nyingine: Chama cha Jubilee Kimesitisha tu Kwa Muda Kumtimua DP Ruto, Tunaomboleza Magufuli: Murathe

Mbunge huyo mtetezi wa chama cha ODM alisema matokeo ya chaguzi ndogo za punde yameonyesha wazi kuwa umaarufu aliodhaniwa kuwa nao Ruto nchini sio kweli.

Akiongea kupitia Citizen TV Jumanne, Machi 23, Wanga alisema kwamba matokeo mabaya ya chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika chaguzi ndogo ni dalili wazi ya kitakachotokea katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.

Wakenya watoa maoni tofauti kuhusu Didmus Barasa kutangaza likizo, kuwazia kumhepa DP Ruto

Alitoa wito kwa wabunge wa Jubilee ambao wamejiunga na chama hicho kipya kujiuzulu nyadhifa zao na kutafuta kura upya ikiwa wana uhakika na umaarufu wa kiongozi wao.

"Uchaguzi mdogo umefichua picha ya kweli kuhusu UDA. Matokeo yanaonyesha kuwa idadi kubwa ya watu wanaolipwa kuja kwenye mikutano ya UDA hakutafsiriki kumaanisha kura. Uwazi umejitokeza. Ninawaomba wabunge waliochaguliwa kupitia tikiti ya Jubilee ambao wamejiunga na UDA kujiuzulu nyadhifa zao na kutafuta kura upya ikiwa wana uhakika na umaarufu wa kiongozi wao," alisema.

Chama hicho kipya, ambacho nembo yake ni Wilbaro, hadi sasa kimeshiriki katika chaguzi ndogo saba na kushinda kiti kimoja tu.

Katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Kabuchai, mgombea wa UDA, Evans Kakai alishindwa na Majimbo Kalasinga wa FORD Kenya kwa tofauti ya kura zaidi ya 1200.

Huko Matungu, chama hicho kipya kiliwakilishwa na Alex Lanya, ambaye aliibuka wa tatu na kura 5,000. Peter Oscar Nabulindo wa ANC alishinda kwa kura 14 257, na David Were wa ODM alifuata na kura 10 565.

Chama hicho pia kilikuwa na wagombea katika wadi nne lakini kiliweza tu kupata kiti cha Wadi ya London.

Katika uchaguzi mdogo uliomalizika hivi punde wa useneta Kaunti ya Machakos, mgombea wa UDA, Urbanus Ngengele alishindwa na Agnes Kavindu wa Wiper na kiasi cha zaidi ya kura 80,000.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Francis M Silva ni Mkuu wa Kitengo cha Kiswahili katika TUKO.co.ke. mwenye tajriba ya miaka mingi katika taaluma ya uwanahabari hasa uhariri - Radio, TV na Mitandaoni. Yeye ni zao la Chuo Anuwai cha Mawasiliano (KIMC). Amefanya kazi katika Radio Umoja, Good News Broadcasting System (GBS TV) na Idara ya Michezo ya Runinga ya Shirika la Utangazaji nchini KBC hadi leo. Hutumia tajriba yake kubwa katika kufanya iwe bora zaidi ya ilivyokuwa.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke