Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ghorofa laporomoka na kuua 12 Misri

Misri Ghorofa Kuporomoka.png Ghorofa laporomoka na kuua 12 Misri

Tue, 18 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

JENGO la ghorofa tano liliporomoka Jumatatu katika mji mkuu wa Cairo, Misri, na kusababisha vifo vya takriban watu 12, mamlaka ilisema, wakati waokoaji wakiendelea kutafuta vifusi.

Kuporomoka kwa majengo ni jambo la kawaida nchini Misri, ambapo ujenzi duni na ukosefu wa matengenezo umeenea katika mitaa ya mabanda, vitongoji duni vya miji na maeneo ya mashambani.

Shirika la habari la serikali la MENA lilisema timu za uokoaji zilitoa miili kutoka kwenye mabaki na kuwapeleka manusura wanne hospitalini kufuatia kuporomoka kwa jengo hilo katika kitongoji cha Hadaeq el-Qubbah, Cairo, takriban kilomita 3.2 kutoka katikati mwa jiji.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live