Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Genge la majambazi lamiminia gari risasi, lamuua dereva

F60c96e8d2e9dfa0 Genge la majambazi lamiminia gari risasi, lamuua dereva

Wed, 23 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mhasiriwa alikuwa ameondoka kwenye barabara kuu ya Thika na kuingia barabara ya Thika wakati genge hilo lilipomvamia Kamanda wa polisi eneo bunge la Juja Dorothy Migarusha alithibitisha kuwa mwathiriwa alipelekwa katika hospitali ya Thika Level Five Hata hivyo, duru zinaarifu kuwa dereva huyo alipoteza maisha yake kutokana na majeraha ya risasiMaafisa wa polisi kaunti ya Kiambu wanachunguza kisa cha kufyatuliwa kwa risasi eneo la Gwa Kairu, mtaani Juja.

Mwasiriwa, dereva ambaye alikuwa akiendesha gari la aina ya Subaru Forester akiwa pekee yake, alikuwa ameondoka tu kwenye barabara ya Kuu ya Thika na kuingia barabara ya Kenyatta wakati genge hilo lilipomvamia.

Kamanda wa polisi eneo la Juja Dorothy Migarusha alithibitisha kuwa mwathiriwa alikimbizwa katika hospitali ya Thika Level Five akiwa mahututi.

Hata hivyo, duru zinaarifu kuwa dereva huyo alipoteza maisha yake kutokana na majerha ya risasi.

Mashuhuda walisema genge la watu watatu waliokuwa wamejihami kwa bunduki na waliokuwa kwenye pikipiki ndio wahusika wakuu wa uhalifu huo.

Gari la mwathriwa lilikuwa na shimo zaidi ya 10 ya risasi.

Kiini cha mauaji hayo hakikujulikana mara moja ingwaje makachrro kutoka Idara ya Upelelezi (DCI) wameanzisha uchunguzi.

Awali, mtangazaji Shiksha Arora alisimulia jinsi alivyoporwa mchana peupe akiendesha gari lake katika mzunguko wa Globe jijini Nairobi.

Kwenye jumbe alizochapisha Twitter, mtangazaji hiyo alisimulia jinsi majamaa watatu walimzubaisha kabla ya kumpora akiwa ndani ya gari lake.

"Jamaa wa kwanza aligonga kioo cha pembeni cha gari langu kukiacha kikiwa kimeinama na kisha akaondoka. Wakati nilikuwa naliteremsha dirisha langu ili kuunda kioo hicho jamaa wa pili alianza kuligonga dirisha la upande wa pili wa gari langu. Wakati nilipogeuka kumuuliza shida ni nini jamaa wa tatu alitumbukiza mkono ndani ya gari na kisha akafungua mlango na kuingia nyuma ya gari langu. Alichukua kipochi changu na akaniamuru nimpe simu yangu," ujumbe wake ulisema.

Arora aliwatahadharisha madereva wengine kutofungua madirisha yao wakipita katika mzunguko huo wa Globe.

Alisema alikuwa na bahati kwani jambazi huyo hakumdhuru licha ya kujairbu kumyonga na kumpora simu na kipochi chake.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka TUKO.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke