Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gavana Obado Afufua Uhasama wake Dhidi ya Raila, Amtolea Makavu

F315ffa63b645c20 Gavana Obado Afufua Uhasama wake Dhidi ya Raila, Amtolea Makavu

Wed, 31 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Okoth Obado alisajili jina lake chini ya chama cha People's Democratic kuzima ushawishi wa ODM

- Alishinda kiti cha ugavana Migori na kuwa gavana wa kwanza wa kaunti hiyo ambayo ni ngome ya ODM

- Mnamo wikendi mwalimu huyo wa zamani alidokezea kuwa atagura ODM na kujiunga na Peoples Democratic Party

Siasa mpya ya kutawala eneo la Nyanza tayari imeanza kuchacha kati ya Gavana Okoth Obado na kiongozi wa ODM Raila Odinga.

Japo hakuna la kutia shaka katika kambi ya ODM, gavana huyo aliashira kwamba atabuni chama kipya na kugura kikosi cha Orange.

Mnamo 2013, Obado alisajili jina lake chini ya chama cha People's Democratic kuzima ushawishi wa ODM na kuwa gavana wa kwanza wa Migori.

Aliwania kiti hicho kupitia tikiti ya chama cha Peoples’ Democratic (PDP) kisichokuwa na umaarufu huku kikosi cha Raila kikimteua profesa Edward Oyugi Akong'o.

Kisha baadaye wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2017, aliwania kiti hicho kupitia tikiti ya ODM.

Hata hivyo, akizungumza Jumapili, Machi 28, Obado alidokezea kuwa atagura ODM hivi karibuni ili kuanzisha chama kipya ambacho kila mtu atawakilishwa.

“Ikiwa watu hao walikuwa wakisema BBI itaunganisha watu, na sisi tunasema kwamba PDP itatuunganisha na kuwezesha watu wetu,” alisema Obado.

Afurahia reggae ya BBI imezimwaKwa mara ya kwanza Obado alionyesha msimamo wake kuhusu Mpango wa Maridhiano (BBI) na rifarenda akisema ni ya kibinafsi.

Alikashifu vigali vigogo wa BBI kupigia debe mageuzi ya katiba wakati taifa linakumbana na janga la kimataifa wengi wakipoteza kazi

“Tunakabiliwa na matatizo mengi katika nchi hii na tuko kati kati ya janga. Tunaumizwa na gharama ya juu ya bei za bidhaa za kimsingi na hali ya maisha imekuwa ngumu,”

“Kwa hivyo, madai kwamba BBI itaimarisha maisha yetu ni uongo mkubwa. Maisha hayawezi kuwa nafuu kutokana na BBI. Tunafurahia kwamba Mungu amesimamisha reggae,”alisema.

Mnamo 2018, wakati alimualika Naibu Rais William Ruto eneo la Kuria Mashariki, gavana huyo ambaye alikuwa ametoka jela baada ya kuzuiliwa kwa siku 34, alimshambulia Raila hadharani.

Lakini haikuwa jambo la kushangaza kwani tayari kulikuwepo fununu kuhusu uhusiano wake wa karibu na Ruto.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke