Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gavana Mandago atangaza kuwania urais 2032 "Mungu atajibu maombi yangu"

A85709e7b93b2f1a Gavana Mandago atangaza kuwania urais 2032 "Mungu atajibu maombi yangu"

Tue, 8 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Gavana Mandago ambaye pia ni mwenyekiti wa Muungano wa Kiuchumi wa Kaunti za Kaskazini Mashariki mwa Bonde la Ufa (NOREB), alisema ana uwezo wa kuongoza taifa hili

- Kiongozi huyo alisema ana rekodi nzuri ya maendeleo katika kaunti ya Uasin Gishu ambayo atatumia kama daraja la kuingia Ikulu

- Babu Owino na Mike Sonko pia wametangaza azma yao ya kuwania urais katika chaguzi za 2027

Gavana wa Uasin Gishu Jackson Mandago ametangaza kuwa atawania urais wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2032.

Mandago ambaye pia ni mwenyekiti wa Muungano wa Kiuchumi wa Kaunti za Kaskazini Mashariki mwa Bonde la Ufa (NOREB), alisema ana uwezo wa kuongoza taifa hili.

Katika video iliyopakiwa na Nation Africa, Mandago alisema ameanza kujiandaa kwa kibarua kinachomsubiri mbeleni na kuweka mipango madhubuti.

"Nina mpango madhubuti. Mwaka 2032, nitakuwa kwenye kinyanganyiro cha urais. Nina miaka 10 ya kujiandaa na kama mjuavyo lizima uwe na mpango. Ninamuomba Mungu anisaidie niwe rais 2032. Muendelee kuniombea Mungu atajibu maombi," alisema Mandago.

Mandago anajiunga na wagombea wengine wa urais ambao wametanga azma yao,

Aliyekuwa gavana wa Nairobi, Mike Sonko alidokezea mnamo Mei kuwa atawania kiti cha urais licha ya kung'olewa mamlakani.

Mwanasiasa huyo alionyesha matumaini kwamba atakuwa kwenye debe wakati wa chaguzi za 2027 na 2032.

"TBT 1, kwa neema ya Mungu na kura zenyu nitakuwa naingia Ikulu mwaka 2027 na 2032," Sonko aliandika kwenye kurasa zake za mtandao wa kijamii.

Hata hivyo, ndoto ya Sonko kuwania urais huenda itakosa kutimia kwani sheria ya Kenya inawazuia viongozi waliotimuliwa mamlakani kuwania viti vya kisiasa.

Mbunge wa Embakasi Babu Owino pia alitangaza kuwa atawania urais baada ya uchaguzi mkuu wa 2017.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke