Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gavana Kinyanjui amfokea DP Ruto, amtaka kukoma kupiga siasa kanisani

7fbde70597d68618 Gavana Kinyanjui amfokea DP Ruto, amtaka kukoma kupiga siasa kanisani

Sat, 26 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Gavana wa Nakuru Lee Kinyanjui alimshutumu DP William Ruto kwa kuwalipa watu wa kumshangilia kanisaniGavana huyo alisema Ruto anakosea heshima hekalu la MunguAliwaambia wanasiasa kutofautisha ibada ya kanisani na mkutano wa kisiasaGavana wa Nakuru Lee Kinyanjui amemwambia Naibu Rais Willam Ruto awache kupiga siasa kanisani.

Gavana Kinyanjui alimshutumu Ruto kwa kuwalipa watu kumshangilia kanisani akiwahutubia waumini, akisema kuwa hatua hiyo ni kukosea hekalu la Mungu heshima.

"Tunapaswa kujua tofauti kati ya ibada ya kanisani na mkutano wa kisiasa kabla ya kuzungumza," Kinyanjui alisema.

Akihutubu akiwa Nakuru Athletics Club wakati wa kumtawaza Askofu David Macharia, Kinyanjui alisema wanasiasa wengi wamegeuza ibada za makanisa kufanya mambo yao wanavyotaka.

"Je, tunaonyesha picha gani kwa wageni ambao wametoka nje ya nchi ambao walikuja kwa shughuli ya kanisa kugeuzwa kuwa uwanja wa kisiasa? Tabia hii ni mbaya sana, na inapaswa kukoma," alisema.

Wakati uo huo, alimwambia mbunge wa Malindi Aisha Jumwa kuwaheshimu watu wa Nakuru, akisema kuwa wana akili na wanajua ni nani wachague kuwawakilisha.

"Kwa Aisha Jumwa, tafadhali waheshimu watu wa Nakuru kwa sababu hatuwezi kufika Malindi na kuwaambia watu wako ni nani wamchague," akaongeza.

Haya yajaniri baada ya Ruto kusema kuwa ameshutumiwa na wengi kwa kujenga makanisa nchini ambapo aliapa kuendelea kuyachangia makanisa.

"Mnajua tayari nimeshtumiwa kuwa mimi ninajenga makanisa, lakini kama unatafuta mtu wa kushirikiana naye, basi nitafute mimi kwa sababu niko tayari," alisema DP Ruto.

Ruto alionekana kumjibu kinara wa ODM Raila Odinga ambaye amekuwa akimshtumu kwa kushiriki michango ya kanisa.

Raila amekuwa akimrushia vijembe Ruto akimtaja kama kiongozi fisadi ambaye anajitajirisha na mali ya umma.

"Kuna hawa ambao wanaiba mali ya umma na kisha wanaanza kuzunguka wakitoa michango kwa kina mama na vijana, harambee kanisani na mabasi kwa shule," alisema Raila wakati wa mazishi ya mfanyibiashara Chris Kirubi.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke