Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gavana Joho, Raila wamchangamkia DP Ruto "Mashujaa Day"

25757f259e58620d Gavana Joho, Raila wamchangamkia DP Ruto Kirinyaga

Wed, 20 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Licha ya tofauti zao za kisiasa vigogo wa kisiasa walionekana wakichangamkiana katika jukwaa Kirinyaga. DP alifika na kuanza kuwasalimia viongozi hao na ilikuwa wazi huenda walikuwa wakitaniana.

Gavana Joho alionekana akiamka akiwa amechangamka na kumsalimia DP huku wakizungumza kwa sekunde kadhaa. Vigogo wa kisiasa leo wameonesha kuweka tofauti za kisiasa kando na kuonekana wakitabasamu baada ya kukutana wakati wa sherehe za Mashujaa Kirinyaga.

Naibu Rais William Ruto alionekana akitabasamu na viongozi ambao hurushiana cheche za maneno kupitia mikutano.

DP alifika kwenye jukwaa katika uwanja wa Wang'uru na kupokea salamu kutoka kwa viongozi waliokuwa wamefika mbele yake.

Walikuwa ni kinara wa ODM Raila Odinga, Gavana Ann Waiguru, Katibu wa Jubilee Raphael Tuju Seneta Gideon Moi, Musalia Mudavadi, Martha Karua baadhi ya wengine.

Licha ya hapo jana kumshambulia Raila akimuita prpject ya serikali katika uchaguzi wa urais 2022, wawili hao walisalimiana na kutabasamu huku wakipeana salamu kwa sekunde kadhaa.



DP pia alionekana kuwa na 'tete-a-tete' na Gavana wa Mombasa Hassan Joho huku wote wawili wakitabasamu.

Joho alimuona DP akiwasalimia viongozi wengine na kumsongea, walisalimiana na kwa sekunde kadhaa wakasemezana.

Huenda wawili hao walikuwa wakitaniana kuhusu ziara za DP ukanda wa Pwani ambapo amekuwa kwa siku kadhaa kupigia debe hustler nation.

Seneta wa Baringo Gideon Moi pia ambaye hujulikana kuwa hasimu wa DP alipata nafasi ya kukutana naye na kusalimiana.

Aidha Ruto pia alionekana kusemezana zaidi na Gavana Waiguru na kiongozi wa Narc Kenya Martha Karua.



Hali hata hivyo ilikuwa tofauti wakati Rais Uhuru Kenyatta aliwasili kwani alimsalia DP kwa haraka na kuenda zake.

Alipofika kwa Raila, walibadilishana salamu zilizoonyesha urafiki wa karibu na kufanya wananchi kushabikia kwa nderemo.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke