Tue, 20 Aug 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mke wa Rais wa zamani wa Namibia, Monica Geingos, ataanza kazi yake mpya kama Chansela katika Chuo cha Kepler kilichopo Kigali, nchini Rwanda, chuo kimesema katika taarifa iliyotolewa jana Jumatatu, Agosti 19.
Monica ambaye ni mfanyabiashara na mwanasheria wa Namibia alihudumu kama Mke wa Rais na Mama wa Taifa wa 3 wa Namibia kutoka 2015 hadi kifo cha mumewe mwaka 2024.
Amekuwa mjumbe wa bodi na mkurugenzi ndani ya kampuni nyingi kubwa za Namibia. Pia alikuwa mwenyekiti wa Baraza la Rais la Ushauri wa Kiuchumi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live