Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Familia ya Samatta ni furaha tu, wachambuzi watoa neno

Samattaa+pic Familia ya Samatta ni furaha tu, wachambuzi watoa neno

Mon, 27 Jul 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

STRAIKA wa Kimataifa, Mbwana Samatta amerejesha furaha katika familia yake, baada ya timu yake ya Aston Villa kubaki kwenye Ligi Kuu England, iliyomaliza nafasi ya 17 na pointi 35.

Wakati shangwe hilo likiendelea kwa Watanzania wengi, Baba mzazi wa staa huyo, Ally Pazi Samatta amefichua ukweli kwamba familia yake ilikosa raha kutokana na mwenendo wa Aston Villa na ilivyobaki waliliamsha shangwe na kushindwa hata kulala.

Mzee Samatta, amesema wakati anatazama mechi ya mwisho ya Aston Villa na West Ham iliyochezwa jana Jumapili, alikuwa na presha kwa kuwa ilibeba hukumu ya timu ya mwanae  kushuka au kubakia ligi kuu.

"Tumeitazama mechi hiyo kwa roho ngumu, kwani tulikuwa hatuna namna, nikaiambia familia yangu tumuombee Mbwana ili afanikiwe kubakiza timu ligi kuu na asionekane kama ameenda na mkosi," amesema.

"Baada ya kupata pointi moja ambayo imewabakiza ligi kuu, ilikuwa kama sherehe kwani hatukulala kwa furaha, tukimshukuru Mungu kusikia maombi yetu," amesema Mzee Samatta.

ALICHOONGEA NA MWANAE

Chanzo: mwanaspoti.co.tz