Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Fahamu umuhimu wa jino la Lumumba

Lumumba Jino Maana.png Fahamu umuhimu wa jino la Lumumba

Mon, 20 Jun 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ubelgiji itamrudishia rasmi Rais Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi, jino ambalo kamishna wa polisi wa Ubelgiji anadai ililitoa kwenye mwili wa Lumumba alipomsaidia kutoweka.

Baada ya kuahirishwa mara kadhaa kwa sababu za kama vile janga la Covid-19 na mipango ya makumbusho, urejeshaji wa jino sasa umepangwa Juni 20.

Watoto wa Lumumba watakuwa sehemu ya ujumbe wa Congo ambao utapokea mabaki hayo, kama sehemu ya hafla binafsi ya kifamilia kama walivyotaka, waziri mkuu wa Ubelgiji alisema katika taarifa yake.

Kwa Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Kongo, Catherine Katsungu Furaha, nchi hiyo ina wajibu wa kurejesha mabaki yamwili wa Patrice Emery Lumumba na kuzika katika ardhi ya Congo ili kuruhusu familia yake ya damu kumaliza maombolezo yaliyodumu kwa miongo kadhaa.

"Ni katika hali hiyo ambapo serikali ya DRC imeungana na familia hiyo ili kujibu ombi lao la kuwapa heshima inayostahili. Kama shujaa wa taifa anahitaji kutambuliwa hivyo", alisisitiza waziri wa utamaduni.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live