Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Fahamu ni kwa nini Hayati Rais wa Tanzania John Magufuli alipewa jina Pombe

4a6f0897c25d01d2 Fahamu ni kwa nini Hayati Rais wa Tanzania John Magufuli alipewa jina Pombe

Tue, 30 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Magufuli alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto 12, alizaliwa na wazazi Joseph Magufuli Marko na Suzanna Ngolo Musa

- Wakati akizaliwa bibi yake au nyanya alikuwa akiandaa pombe na akampa jina Walwa, ambalo kwa lugha ya Kisukuma kule Tanzania ni Pombe

- Kwa jumla viongozi 17 kutoka Afrika walikuwa wamethibitisha kuhudhuria mazishi ya kiserikali ya Rais wa zamani wa Tanzania, msemaji mkuu wa serikali Hassan Abbasi alisema kwenye hotuba yake

- Magufuli aliagwa na hatimaye kuzikwa kiserikali kwenye makaburi ya familia nyumbani kwao Chato Ijumaa Machi 26, 2021 kwenye hafla iliyohudhuriwa na maelfu ya watu

Marehemu Rais John Pombe Magufuli alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto 12, alizaliwa na wazazi Joseph Magufuli Marko na Suzanna Ngolo Musa.

Wakati alipozaliwa bibi yake au nyanya alikuwa akiandaa pombe na akampa jina Walwa, ambalo kwa lugha ya Kisukuma kule Tanzania ni Pombe. Ndivyo hivyo Rais wa awamu ya tano alivyoitwa jina Pombe.

Magufuli aliagwa na hatimaye kuzikwa kiserikali kwenye makaburi ya familia nyumbani kwao Chato Ijumaa Machi 26, 2021 kwenye hafla iliyohudhuriwa na maelfu ya watu.

Rais Uhuru Kenyatta ni miongoni mwa viongozi wa mataifa mbalimbali waliosafiri kwenda Tanzania kutoa pole zao kabla ya kuzikwa kwa rais huyo. Pia Lazaro Chakwera wa Malawi, Edgar Lungu wa Zambia vilevile Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo na Makamu wa Rais wa Burundi Prosper Bazombanza walifika.



Wengine waliofika Dodoma binafsi kutoa pole zao ni marais wa Visiwa vya Comoro Azali Assoumani, Mokgweetsi Masisi wa Botswana, Filipe Nyusi wa Msumbiji, na Matamela Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini.

Marais wa Rwanda, Angola na Burundi waliwakilishwa na maafisa wa ngazi za juu.

Kwa jumla viongozi 17 kutoka Afrika walikuwa wamethibitisha kuhudhuria mazishi ya kiserikali ya Rais wa zamani wa Tanzania, msemaji mkuu wa serikali Hassan Abbasi alisema kwenye hotuba yake.

Magufuli anasifiwa kwa vita vyake dhidi ya rushwa na maendeleo makubwa aliyoweka katika miradi ya miundombini, lakini wakosoaji wake wamemtaja kuwa kiongozi aliyekandamiza demokrasia, uhuru wa wanahabari, watetezi wa haki za binadamu na upinzani.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke