Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Félix Tshisekedi aonya mtafaruku wa maaskofu

Tshisekedi Aonya Mtafaruku Wa Maaskofu Félix Tshisekedi aonya mtafaruku wa maaskofu

Mon, 26 Jun 2023 Chanzo: Bbc

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Félix Tshisekedi ameonya "mtafaruku" katika kanisa katoliki ambao unahatarisha umoja wa kitaifa kabla ya uchaguzi wa rais.

Wiki iliyopita, maaskofu wa DRC waliwataka watu wa Congo kuwa macho kwa ajili ya uchaguzi wa kuaminika.

Akijubu maaskofu moja kwa moja, Bw Tshisekedi alisema kuwa katika uongozi wa kanisa la eneo kuna “mtafaruku ambao ningeuelezea kuwa hatari, haswa katika mwaka huu wa uchaguzi."

"Miongoni mwenu, kwa bahati mbaya kuna watu wachache ambao wamechukua mwelekeo hatari ambao unaweza kuligawa taifa letu ... siwezi kukubaliana na jambo kama hilo", aliongeza baada ya misa ya Jumapili katika maadhimisho ya miaka 50 ya Askofu wa Mbuji-Mayi Emmanuel-Bernard Kasanda katikati ya Congo.

Katika taarifa yao wiki iliyopita, maaskofu wa kanisa katoliki DRC walisema, "hali ya kisiasa ni ya wasiwasi" na kuchukiza, "ukandamizaji mbaya zaidi wa upinzani, vikwazo vya uhuru, ukandamizaji wa haki na watu kukamatwa kiholela" tangu Bw Tshisekedi achukue hatamu mwaka wa 2019.

"Kwa uchaguzi wa kuaminika, watu wa Congo, kuweni macho!”, Maaskofu waliwaambia wenzao.

Chanzo: Bbc