Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ethiopia yasaini mkataba na Somaliland ili iweze kutumia bahari

Ethiopia Yasaini Mkataba Na Somaliland Ili Iweze Kutumia Bahari Ethiopia yasaini mkataba na Somaliland ili iweze kutumia bahari

Tue, 2 Jan 2024 Chanzo: Bbc

Ethiopia imechukua hatua za kwanza za kisheria katika mwelekeo ambao siku moja itaiwezesha nchi hiyo isiyo na bahari kupata ufikiaji wa bahari, serikali yake inasema.

Nchi hiyo imetia saini kile kinachojulikana kama mkataba wa maelewano (MoU) na jamhuri iliyojitangaza kuwa ya Somaliland, kutumia mojawapo ya bandari zake.

Awali, Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed alielezea upatikanaji wa bahari ni suala linalowezekana kwa nchi yake.

Katika hotuba yake ya mwezi Oktoba ambayo ilizua hofu katika nchi hiyo - wananchi walidhani hatua hiyo itakuwa ni kujaribu kuchukua ardhi kutoka kwa nchi jirani ya Ethiopia, ambayo ni Eritrea.

Makubaliano yaliyoafikiwa siku ya Jumatatu na Somaliland hayajawekwa wazi lakini taarifa kutoka ofisi ya Abiy ilisema "itafungua njia ili kutimiza azma ya Ethiopia kupata ufikiaji wa bahari".

Mazungumzo hayo yamelenga bandari ya Somaliland ya Berbera.

Mshauri wa masuala ya usalama wa taifa, Redwan Hussien alisema kwenye ukurasa wa X kwamba makubaliano hayo yataiwezesha Ethiopia kukodishwa eneo la kijeshi lililopo baharini.

Mkataba huo haupo kisheria lakini unaashiria ushindi mkubwa wa kidiplomasia kwa Addis Ababa.

Akizungumza wakati wa utiaji saini, Rais wa Somaliland, Muse Bihdi Abdi alisema makubaliano hayo yanajumuisha Ethiopia kuitambua Somaliland kama nchi huru katika siku zijazo.

Somaliland imejitenga na Somalia kwa zaidi ya miaka 30 sasa lakini haitambuliwi na Umoja wa Afrika (AU) wala Umoja wa Mataifa kama taifa huru.

Hapakuwa na majibu kuhusiana na tangazo hilo kutoka Somalia, ambayo inaichukulia Somaliland kama sehemu ya eneo lake. Lakini shirika la utangazaji la kitaifa SNTV limeripoti kuwa kutakuwa na kikao cha dharura cha baraza la mawaziri siku ya Jumanne kujadili suala hilo.

Ethiopia taifa la watu milioni 100, ni moja ya taifa lenye idadi kubwa ya watu miongoni mwa mataifa yasiyo na bahari.

Chanzo: Bbc