Jeshi la ulinzi nchini Ethiopia limezindua silaha za kivita za anga na nchi kavu zitakazo tumika kuwadhibiti waasi wa Tigray waliopo katika mkoa wa Amhara kaskazini mwa Ethiopia.
Nae Msemaji wa chama cha Tigray People's Liberation Front TPLF kinachoongoza eneo hilo, Getachew Reda, amesema kuwa waasi hao wamepokea mashambulizi ya anga yaliyotekelezwa kwa silaha za moto siku hache zilizopita.
"Vikosi vya jeshi vimeimarishwa vilivyo, hatuna hakika ni wapi vikosi hivyo vitaanza kufanya mashambulizi" amesema Getachew.
Chama cha TPLF kimesema kuwa mashambulizi hayo mapya yameanza toka Oktoba 7, 2021, na tayari yameshafanyika katika maeneo matatu yaliyopo mkoani hapo.
Hata hivyo inaelezwa kuwa kwa takribani wiki chache zilizopita hakukuwa na mashambulizi ya aina yoyote kwa pande zote mbili.