Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ethiopia: Mapigano yazuka katika mpaka wa Tigray na Amhara

Ethiopia: Mapigano Yazuka Katika Mpaka Wa Tigray Na Amhara Ethiopia: Mapigano yazuka katika mpaka wa Tigray na Amhara

Tue, 16 Apr 2024 Chanzo: Bbc

Mapigano yamepamba moto katika moja ya maeneo yanayozozaniwa kati ya majimbo ya Tigray na Amhara nchini Ethiopia katika kipindi nadra cha vurugu baada ya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwishoni mwa 2022 kumaliza moja ya vita mbaya zaidi barani Afrika.

Wilaya ya Raya Alamata- inayozozaniwa na majimbo yote mawili- ilikuwa chini ya Tigray kusini kabla ya vita kuanza lakini tangu wakati huo imekuwa chini ya udhibiti wa vikosi vya Amhara.

Wakazi waliambia BBC kwamba mapigano yalianza wikendi na kuendelea kwa siku kadhaa.

Maafisa wa Amhara waliwashutumu wapiganaji wa kundi la Tigray Peoples Liberation Front (TPLF) kwa kuanzisha mashambulizi huku mkuu wa eneo la Kusini mwa Tigray akisema wanamgambo wa Amhara walifyatua risasi.

Chama cha upinzani cha National Movement of the Amhara (NaMA) katika taarifa kililaumu TPLF ambayo ilisema ilikuwa ikianzisha "uvamizi."

Akiandika kwenye X, Getachew Reda- mkuu wa utawala wa muda wa Tigray, aliyeanzishwa baada ya makubaliano ya amani- alisema "maendeleo" ya hivi karibuni katika maeneo hayo hayakuhusisha migogoro kati ya vikosi vya Tigray na serikali ya shirikisho au kati ya mikoa jirani ya Tigray na Amhara.

Alilaumu "maadui" wa mpango wa amani "kutoka karibu au mbali" kwa matukio bila kutaja wao ni nani.

Haijabainika kama kuna majeruhi wowote lakini vyombo vya habari vinavyounga mkono Amhara viliripoti kwamba vikosi vya Tigray viliingia katika baadhi ya wilaya siku ya Jumatatu.

Hivi majuzi serikali ya shirikisho imesema jeshi litadhibiti maeneo yenye migogoro hadi suluhu litakapotolewa.

Kuna wasiwasi kwamba hii inaweza kuzidisha mzozo unaoendelea tangu Agosti mwaka jana katika eneo la Amhara- Ethiopia lenye watu wengi zaidi- kati ya wanamgambo wa ndani na jeshi.

Chanzo: Bbc