ESTONIA inapanga kufungua ubalozi wake katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi mwakani.
Ubalozi huo utakuwa ni wa pili wan chi hiyo barani Afrika, wa kwanza ukiwa nchini Misri ambao umekuwa ukifanya kazi tangu 2010.
Mpango wa kufungua ubalozi huo mpya ulibainishwa katika mpango Estonia kwa Afrika katika kipindi cha 2020-2030.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya inakusudia kusaidia wanadiplomasia wa Estonia katika kugombea huduma ya mambo ya nje katika Jumuiya ya Ulaya barani Afrika, kuimarisha ubadilishanaji wa wanadiplomasia na nchi nyingine wanachama na kuongeza ushiriki wa Estonia barani Afrika.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Estonia pia inakusudia kupanua mtandao wa mabalozi wa heshima katika nchi za Kiafrika.
Katika nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, mabalozi wa nchi hiyo ambao sio raia wa Estonia wameteuliwa katika nchi za Ethiopia na Mali.