Wed, 18 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Elias Mpedi Magosi, Kutoka Botswana amechaguliwa kuwa Katibu Mtendaji Mpya wa SADC akichukua nafasi hiyo kutoka kwa Mtanzania Dkt. Stergomena Lawrence Tax.
Mpaka anachaguliwa kushika wadhifa huo Magosi pia ni Mkuu wa Utumishi wa Umma na Katibu wa Baraza la Mawaziri wa Botswana
Magosi sio mgeni ndani ya SADC, amewahi kuhudumu nafasi ya Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala wa Sekretarieti ya SADC, Machi 2017 hadi April 2018.
Kiapo cha Magosi kinamaliza utawala wa miaka 8 Dkt. Stergomena Tax ambaye amemaliza muda wake wa kuiongoza SADC kwa vipindi viwili
Chanzo: www.tanzaniaweb.live