Fri, 17 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Maafisa wa afya wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wametangaza kudhibitiwa kwa wimbi la kumi na tatu la ugonjwa wa Ebola, ambapo watu 11 waliugua huku sita wakifariki dunia.
Maambukizi hayo yalitokea mwezi Oktoba mwaka huu katika eneo la Beni, kwenye jimbo la North Kivu Mashariki mwa Jamhuri hiyo.
Wimbi hilo lilizua hofu na taharuki kwa wananchi wa DRC, kwa mara ya kwanza ugonjwa huo uliingia DRC mwaka 2018 na 2021 kusababisha vifo vya takribani watu 2,300.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live