Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za magharibi mwa Afrika, Ecowas imeweka vikwazo dhidi ya viongozi wa mpito wa Mali na familia zao.
Vikwazo vinaanzia marufuku ya kusafiri hadi kufungia mali zao za kifedha.
Hatua hii imekuja baada ya kushindwa kwao kuzingatia ratiba ya kurejesha nchi kwenye utawala wa kikatiba ifikapo Februari mwaka ujao.
Ecowas ilisema kuwa mamlaka ya Mali iliwafahamisha kuhusu kutoweza kwao kufikia makataa ya mpito ya kufanya uchaguzi.
Jumuiya hiyo ilikuwa imeondoa vikwazo vya kiuchumi vilivyowekewa nchi hiyo kutokana na mapinduzi ya mwaka jana baada ya jeshi kuahidi mchakato wa mpito wa miezi 18.
''Ecowas itazingatia vikwazo zaidi mwezi ujao ikiwa bado hakuna maendeleo kuelekea uchaguzi nchini Mali'', ilisema.
Mali imeshuhudia mapinduzi mara mbili tangu mwaka jana na iko katika mtego wa waasi wa kijihadi.