Jumuiya ya kiuchumi wa nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS, imetilia mashaka mwenendo wa uchaguzi mkuu nchini Mali kufuatia kupelekwa mbele kufuatia mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika mwaka jana 2021.
Katika taarifa iliyotolewa na Jumuiya hiyo, imesema kuwa mwenendo wa uchaguzi nchini humo hautoi matumaini kwani hadi sasa hakuna maandalizi thabiti ya kupiga kura.
Hata hivyo tarifa hii imetolewa mara baada ya Rais msataafu wa Nigeria Goodluck Jonathan, kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini humo.
Mapema mwezi Julai, Serikali ya mpito ilitangaza kufanya chaguzi huo ikiwa ni hatua ya kurejesha Serikali huru yenye demokrasia na usawa.