Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

ECOWAS yakaza uzi tawala za kijeshi

ECOWAS UZI ECOWAS yakaza uzi tawala za kijeshi

Sat, 5 Feb 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Jaribio la mapinduzi nchini Guinea Bissau lilikuwa tukio jingine la karibuni kabisa kwenye kanda ya Afrika Magharibi ambayo inaandamwa na visa vya wanajeshi kuziondoa kwa nguvu madarakani serikali za kiraia.

Jumuiya ya ECOWAS imejitwika dhima kubwa kwa kuyachukulia hatua nzito mataifa yalifanya mapinduzi na imerejea msimamo wake wa kupinga wanajeshi kutwaa madaraka.

Jean-Claude Kassi Brou ni rais wa Halmshauri Kuu ya Jumuiya ya ECOWAS na amesema "Hali hii, hali ya usalama siyo sababu ya jeshi kuchukua madaraka. Kazi ya jeshi ni kulinda mipaka na kupambana na shughuli za kigaidi. Kwa sababu taathira za mapinduzi haya ni kupungua kwa uungaji mkono wa jumuiya za kikanda na kimataifa hususan katika mapambano dhidi ya ugaidi"

Hadi sasa ECOWAS imesitisha uanachama wa mataifa matatu ya Mali, Guinea na Burkina Fasso kutokana na mapinduzi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live