Arusha. Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) leo Jumatano Aprili 15, 2020 imetoa msaada wa maabara zinazotembea kwa nchini wanachama kwa ajili ya kupima virusi vya corona.
Maabara hizo zipo katika magari, Tanzania imepatiwa magari mawili sawa na Kenya na Uganda huku Rwanda, Burundi na Sudan Kusini kila nchi ikipatiwa gari moja.
Lengo la maabara hizo ni kuongeza kasi ya upimaji wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya corona.
Katibu mkuu wa EAC, Balozi Liberati Mfumukeko ametoa taarifa hiyo leo Jumatano Aprili 15, 2020 makao makuu ya jumuiya huyo jijini Arusha na kueleza pia wametoa vifaa kinga kwa watoa huduma
"Maabara moja inatumia magari mawili kwa ajili ya vifaa mbalimbali na kukaa maafisa wa afya," amesema
Mkuu wa kitengo cha afya wa EAC, Michael Katende amesema maabara hizo tisa zina thamani ya dola 1.8 milioni ambazo ni zaidi ya Sh3.6 bilioni.
Habari zinazohusiana na hii
- Bila barakoa hakuna kuingia KCMC
- Wagonjwa wapya sita wa corona wabainika Zanzibar, mmoja afariki dunia
Amesema maabara hizo licha ya kupima corona kwa wakati pia zitaweza kupima magonjwa mengine ya mlipuko kama Ebola.
Magari hayo yameondoka leo makao makuu ya jumuiya hiyo kwenda katika nchi wanachama na yatapokelewa mipakani na serikali husika.