Wed, 29 Sep 2021
Chanzo: Jamii Forums
Diwani Mstaafu wa Wadi ya Kiptoror, Barnaba Lagat anadaiwa kuwa na hali mbaya Kiafya katika Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya Moi iliyopo Eldoret baada ya Afisa wa Polisi kumpiga risasi kifuani.
Diwani huyo aliachwa akivuja Damu nyingi baada ya kupigwa risasi kwa kutovaa Barakoa majira ya jioni akiwa Kituo cha Biashara cha Kapsigilai.
Daniel Chebet ambaye alishuhudia kisa hicho ameiambia K24 Digital kwamba Afisa aliyempiga risasi Lagat alikuwa amelewa na inadaiwa alitumia nguvu nyingi kutekeleza Maagizo ya Wizara ya Afya katika kuzuia .
Chanzo: Jamii Forums