Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dereva Mlevi wa Ambulensi Ahusika Kwenye Ajali, Wagonjwa Wajeruhiwa

9eb55c6eb07daa62 Dereva Mlevi wa Ambulensi Ahusika Kwenye Ajali, Wagonjwa Wajeruhiwa

Mon, 12 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Dereva huyo alikuwa amepiga mtindi na akashindwa kulidhibiti gari hilo la wagonjwa

- Kisa hicho kimekashifiwa huku shirika la Msalaba Mwekundu likitakiwa kuchukua hatua kali dhidi ya matumizi ya magari ya wagonjwa

- Dereva huyo atafikishwa mahakamani Jumatatu Aprili 12

Wagonjwa kadhaa walijipata pabaya baada ya dereva wa ambulensi ya Shirika la Msalaba Mwekundu kuingia kazini akiwa amepiga mtindi.

Ripoti zinaarifu kuwa dereva huyo mtundu alikuwa na wagonjwa kwenye ambulensi hiyo waliokuwa wakikimbizwa hospitali ya Kabarnet Kaunti ya Baringo.

Athari za kinywaji alichokuwa amebugia zilimfanya kushindwa kulidhibiti gari hilo na hivyo kupoteza mwelekeo.

Ililazimu wagonjwa hao kuokolewa kutoka ajali hiyo na kukimbizwa hospitalini wakiwa na maumivu zaidi.

Dereva huyo alikamatwa na maafisa wa polisi wa kituo cha Kabarnet na kuzuiliwa akisubiri kushtakiwa Jumatatu Aprili 12.

Kisa hicho kilikashifiwa vikali huku wahudumu wa bodaboda wakisema magari ya kukimbiza wagonjwa hospitali yamekuwa yakitumiwa vibaya.

Mnamo mwezi Aprili 2020, Wakenya walibaki kinywa wazi baada ya afisa wa shirika la Msalaba Mwekundu kumuagiza dereva atumie ambulensi kumpeleka mwanawe nyumbani pamoja na rafiki zake.

Watoto hao walionekana wakijivinjari kwa vinywaji ndani ya gari hilo la kuwabeba wagonjwa walio katika hali mahututi.

Kelele za Wakenya zilifanya shirika hilo kumsimamisha kazi afisa huyo aliyehusika katika kisa hicho.

Kufikia alasiri, shirika hilo jata hivyo halikuwa limesema lolote kuhusu kisa hicho cha Jumamosi Aprili 10.

Wakati uo huo, abiri waliokuwa wakisafiria matatu moja walinusurika kifo katika barabara ya Nakuru-Ravine katika makutano ya barabara ya Aic Moi Academy.

Matatu hiyo iligongana na gari moja la kibinafsi Jumapili Aprili 11 asubuhi.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke