Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DRuto asema Raila alaumiwe kusambaratika kwa Jubilee

26bd79278e509031 DRuto asema Raila alaumiwe kusambaratika kwa Jubilee

Sat, 6 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Naibu Rais William Ruto amemlaumu kinara wa ODM Raila Odinga kutokana na kufeli kutekelezwa kwa ahadi ambazo utawala wa Jubilee uliwapa Wakenya katika uchaguzi wa 2017.

Kiongozi huyo aliwataka vijana kumuunga mkono katika uchaguzi ujao ili aweze kufufua Ajenda Nne Kuu kupitia mfumo wake wa kujenga uchumi kuanzia chini kuelekea juu.

Ruto alidai kuwa kila kitu kilipangwa vyema hadi pale Raila “aliteka nyara” mpango wa serikali alipowasilisha Mchakato wa BBI.

Akizungumza alipozuru kaunti ya Bungoma, Ruto alidai kuwa kila kitu kilipangwa vyema hadi pale Rala “aliteka nyara” mpango wa serikali kwa alipowasilisha Mchakato wa Kurekebisha Katiba (BBI).

"Kila kitu kilipangwa vyema hadi Raila alipoingia Jubilee na kuanzisha mpango wa kurekebisha Katiba chini ya BBI. Ni wakati huu ambapo ajenda ya serikali ikiwa ni pamoja na Ajenda Nne Kuu ikiwemo mpango wa kuwapa ajira vijana ulipotumbukia," Ruto alisema.

Kiongozi huyo aliwataka vijana kumuunga mkono katika uchaguzi ujao ili aweze kufufua Ajenda Nne Kuu kupitia mfumo wake wa kujenga uchumi kuanzia chini kuelekea juu.

"Tutafufua Ajenda Nne Kuu kwa kupitia mfumo wa kujenga uchumi kutoka chini kuelekea juu. Uchumi wetu umekuwa unaodorora na pindi tu nitakapoingia afisini katika wmake mwangu wa kwanza nitakuwa nashughulikia swala hilo," alisema.

Katika mikutano yake ya hadhara, pia alimkosoa Raila na wapinzani wake wengine anapoazimia kuwania urais. Alisema pamoja na kwamba washindani wake wameshika nyadhifa za juu zaidi na wamekaa kwenye siasa muda mrefu zaidi yake, hawana rekodi ya maendeleo inayoonekana.

"Wameshikilia nyadhifa za waziri mkuu, makamu wa rais na naibu waziri mkuu ilhali hawana la kuonyesha, tofauti na mimi ambaye nimefanya mengi wakati wa utawala wangu kama DP katika serikali ya Jubilee," DP alidokeza.

Ruto aliwarai wenyeji wa kutoka Magharibi mwa Kenya kumpigia kura akisema kuwa ana nafasi nzuri zaidi ya kushinda uchaguzi huo ikilinganishwa na washindani wanaotoka eneo hilo.

Alisema kwa sasa chama chake cha UDA kinaungwa mkono na wabunge zaidi ya mia moja nchi

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke