Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DRC: Umoja wa Mataifa waanza kuondoa kikosi chake MONUSCO

DRC: Umoja Wa Mataifa Waanza Kuondoa Kikosi Chake MONUSCO DRC: Umoja wa Mataifa waanza kuondoa kikosi chake MONUSCO

Wed, 28 Feb 2024 Chanzo: Bbc

Umoja wa Mataifa umeanza kuondoa vikosi vya kulinda amani vya MONUSCO Jumatano kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa kukabidhi kituo cha kwanza cha Umoja wa Mataifa kwa polisi wa kitaifa, AFP imeshuhudia.

Wakati wa sherehe rasmi katika kambi ya Kamanyola, karibu na mipaka ya Rwanda na Burundi, bendera za Umoja wa Mataifa na Pakistan, nchi za asili za walinda amani wanaosimamia amani zilibadilishwa na zile za DRC.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetaka kuondolewa kwa wanajeshi hao licha ya wasiwasi wa Umoja wa Mataifa kuhusu ghasia zilizokithiri mashariki mwa nchi hiyo.

Kinshasa inalichukulia jeshi la Umoja wa Mataifa kama lisilo na ufanisi katika kuwalinda raia dhidi ya makundi yenye silaha na wanamgambo ambao wamepiga mashariki mwa nchi hiyo kubwa kwa miongo mitatu.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga kura mwezi Disemba ili kuharakisha matakwa ya Kinshasa ya kutaka kuondolewa kwa taratibu kwa ujumbe wa MONUSCO, ambao uliwasili mwaka 1999.

Kikosi cha Umoja wa Mataifa kwa sasa kina wanajeshi 13,500 na polisi 2,000 katika majimbo matatu ya mashariki ya Ituri, Kivu Kusini na Kivu Kaskazini.

Kabla ya mwezi Mei, kikosi cha Umoja wa Mataifa kitaondoka katika kambi zake 14 katika jimbo hilo na kuvikabidhi kwa vikosi vya usalama vya DRC.

Chanzo: Bbc