Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DRC: Ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi kutoka EU waahirishwa

DRC: Ujumbe Wa Waangalizi Wa Uchaguzi Kutoka EU Waahirishwa DRC: Ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi kutoka EU waahirishwa

Thu, 30 Nov 2023 Chanzo: Bbc

Serikali ya DRC imesikitishwa na uamuzi wa EU kuuondoa Ujumbe wake wa waangalizi nchi nzima.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari kupitia X iliyochapishwa jana, msemaji wa Serikali alieleza kuwa kuahirishwa huko kulikuja wakati wataalamu wa Serikali na Umoja wa Ulaya walipokuwa kwenye mazungumzo kuhusu kupelekwa kwa misheni hiyo nchi nzima.

EU nchini DRC ilitangaza kughairi kupitia mtandao wa X ikisema kuwa kutokana na vikwazo vya kiufundi vilivyo nje ya uwezo wa EU, Ujumbe huo ulilazimika kufuta ujumbe wa waangalizi wa uchaguzi wa EU katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Ujumbe wa EU ulikuwa umepanga kupeleka waangalizi wa muda mrefu katika majimbo mengi ya DRC, lakini hili halikuwezekana tena.

Tume Huru ya Kitaifa ya Uchaguzi itafunga uidhinishaji wa Waangalizi wa Uchaguzi tarehe 5 Desemba 2023, majadiliano yanayoendelea kati ya EU na serikali ya DRC hayazuii uwepo wa wataalamu kadhaa wa uchaguzi wa Umoja wa Ulaya.

Ujumbe wa EU hapo awali ulialikwa na serikali ya Congo. Tarehe 20 mwezi Desemba 2023, DRC itafanya uchaguzi wake wa 4 wa urais, pamoja na ubunge katika ngazi ya kitaifa na majimbo, tangu kuanzishwa upya kwa utawala wa kidemokrasia mwaka 2006.

Chanzo: Bbc