Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wakimbizi katika kambi kubwa ya Kanyaruchinya huko Nyiragongo wanakabiliana na hali ngumu ya maisha kwenye mahema wanakoishi baada ya kukimbia makaazi yao kutokana na utovu wa usalama. Hillary Ingati alitembelea kambi hiyo na kuzungumza na baadhi ya wakimbizi hapa….
Kilomita 18 kutoka katika mji mwa Goma, tunawasili katika kambi hii, pembezoni mwa mlima wa Volcano.
Maelfu ya watu, wengi wao wanawake na watoto wanaishi ndani ya mahema ambayo yanaonekana kuwa madogo kukidhi idadi ya kila familia.
Baadhi ya mahema hayo, yamechanika. Wakimbizi wanaoshi hapa, wanaonekana kudhoofika kiafya. Nazungumza na mama huyu.
Aidha mama huyu anatuelezea wasiwasi wake.