Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto kuzuru ngome ya Raila Odinga kupigia upato

96f185dad267697c DP Ruto kuzuru ngome ya Raila Odinga kupigia upato

Tue, 15 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Edward Owalo alisema Naibu Rais William Ruto atazuru mkoa wa Nyanza kati kati ya mwezi Julai mwaka huuOwalo aliongezea kwamba ziara ya Ruto itahusisha uzinduzi wa miradi ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake na vijanaRuto pia atafanya mikutano ya faragha na vikundi vya wanawake na vijanaNaibu Rais William Ruto anatarajiwa kuzuru mkoa wa Nyanza ambao unaaminika kuwa ngome ya hasidi wake mkuu wa kisiasa Raila Odinga.

Kwa mujibu wa taarifa za The Standard, Owalo alisema Ruto atafanya ziara hiyo kati kati mwa mwezi Julai mwaka huu ambapo atazindua miradi kadhaa ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake na vijana.

Ruto pia atafanya mikutano ya faragha na vikundi kadhaa vya wanawake na vijana, atahudhuria mikutano makanisani ikiwa ni njia moja wapo ya kupigia upato Huster Nation eneo hilo.

" Mashauriano kati ya washikadau wahusika wa hustler nation yanaendelea, na ratiba kamili itatolewa hivi karibuni," Owalo alisema.

Ruto ataanzia ziara yake kaunti ya Migori alafu atafululiza hadi Kisumu, kisha baadaye kuzuru kaunti za Homa Bay na kumalizia Siaya.

Katika sherehe za kuadhimisha siku kuu ya Madaraka mwaka huu, Ruto alipokelewa vema na wakazi wa Kisumu na anaamini hiyo ilikuwa ishara ya kuonyesha kwamba ana wafuasi eneo hilo.

Owalo ambaye alikuwa mwandani wa Raila na akamtema, alidai kwamba ziara ya Ruto mkoani Nyanza itabadilisha siasa ambazo kwa miaka mingi mkoa huo umetawaliwa na chama cha ODM.

Ruto anatazamia kumrithi Rais Uhuru Kenyatta ambaye muhula wake unakamilika mwaka wa 2022 ambapoa atakuwa ameongoza taifa kwa miaka 10.

Viongozi kadhaa wametangaza azma ya kuwania kiti hicho akiwemo, Mukhisa Kituyi, Musalia Mudavadi, gavana wa Mombasa Hassan Joho na wengineo.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke