Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto azidi kubanwa, wafuasi wasubiri kuona ujanja wake

97f84a86baa54150 DP Ruto azidi kubanwa, wafuasi wasubiri kuona ujanja wake

Fri, 13 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Ijumaa Agosti 13 yameangazia taabu anayopata Naibu wa Rais William Ruto katika juhudi zake za kutafuta kura za Mt Kenya katika safari yake ya kuingia Ikulu.

Baadhi ya viongozi wa eneo hilo wanasisitiza ni lazima waunde vyama vyao kabla ya kufanya mjadala wowote na kile cha DP cha UDA.

1. Star

Jarida hili limeangazia kikao cha Mbunge Moses Kuria, aliyekuwa waziri Mwangi Kiunjuri na kiongozi wa NARC Kenya Martha Karua Alhamisi Agosti 12.

Watatu hao walikutana Limuru na kutangaza kuwa wanataka kuunda muungano wa Mt Kenya ambao utatetea maslahi ya eneo hilo.

Walisema ni baada ya kuwa na muungano huo ambapo watafanya mazungumzo kuhusu watakayemuunga mkono 2022.

Mhariri pia ameangazia taarifa za majonzi ambapo ndugu wanne waliangamizwa baada ya kushukiwa kuwa wezi wa mifugo kaunti ya Kajiado.

2. People Daily

People Daily imeangazia siasa za 2022 ambapo viongozi waliotimuliwa afisini kwa tuhuma za ufisadi wako na nafasi ya kuwania viti tena.



Read also

"Mengi Yanakuja": Moses Kuria Asema Baada ya Kukutana na Kiunjuri, Martha Karua

EACC ilisema haina uwezo wa kuwazuia washukiwa hao kuwania viti kwani sheria imewapa mwanya wa kufanya hivyo licha ya tuhuma zinazowakabili.

Mwenyekiti wa EACC Twalib Mbarak alisema ni baada ya kesi tu kukamilika na mshukiwa kupatikana na hatia ambapo wanaweza kumzuia kuwania kiti.

3. Standard

Mhariri wa gazeti hili amezua maswali kuhusu anachopanga DP Ruto kwenye siasa za 2022 baada ya mdosi wake kumtema.

Ni wazi sasa kuwa Rais Uhuru Kenyatta hamtaki karibu na Ikulu na badala yake akaamua kumuunga mkono Raila Odinga kuendeleza ajenda zake baada ya kuondoka 2022.

Kuna taarifa pia kuhusu ndugu wanne waliouawa kinyama Kajiado baada ya kushukiwa kuwa wezi wa mifugo.

Wanne hao ni Freddie Wanjiru, 30, na nduguye Victor Wanjiru, 25 pamoja na binamu wao Mike George, 29, na Nicholas Musa, 28.

Wanne hao walikuwa wametoka Syokimau kuenda bash ya rafiki wao Isinya Jumapili Agosti 8 na walipokuwa wakirudi Jumatatu Agosti 9 wakashambuliwa na wakazi.

Taifa Leo

Mhariri wa Taifa Leo ameangazia athari za maradhi ya Covid-19 ambapo familia nyingi zinalia vifo vya wapendwa wao.

Aidha kuna taarifa pia kuhusu kizungumkuti cha 2022 baada ya Rais Kenyatta kushindwa kushawishi viongozi wa muungano wa OKA kumuunga mkono Raila Odinga.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke