Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto awazomea Rais Uhuru na Raila: Wachaneni na katiba

4b3b031d0ebc82e9 DP Ruto awazomea Rais Uhuru na Raila: Wachaneni na katiba

Fri, 11 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- DP anaendelea kuzua uhasama kati yake na Rais huku akipuuza wito wa kufanyia katiba marekebisho

- Alisema suluhu la matatizo ya Kenya ni mfumo anaopendekeza wa kiuchumi ambapo kila Mkenya atakuwa na nafasi ya kujijenga

- Rais na Raila wamekuwa wakiendesha kampeni za kufanyia katiba marekebisho kama suluhu la uhasama wa kila mwaka wa uchaguzi

- DP hata hivyo anasema hizo ni fikra za viongozi wakabila wanaotaka kujizawadia nyadhifa za uongozi

Naibu William Ruto amekiri kuwepo tofauti kuhusu barabara ambayo Kenya inafaa kufuata katika kutatua masaibu yake.

Ruto alisema wenzake wanataka kubadilisha katiba kutatua masuala ilhali suluhu kamili ni kubadili mfumo wa kiuchumi nchini.

“Kuna mgawanyiko kubwa kati yetu ambao tunafikiria kuwa masaibu ya Kenya ni ya kiuchumi ambayo yanaweza kusuluhishwa na mfumo mpya wa kiuchumi utakaohakikisha kila nafasi inaundwa kwa kila Mkenya kupata kazi au kufanya biashara," alisema Ruto.

Alisema juhudi ambazo zimekuwepo za kubadili katiba zinaongozwa na fikra za kikabila ambapo vigogo wanataka kujizawadi.



“Wale wengine wanafikiria shida ya Kenya ni ukabila na suluhu ni kuunda nafasi za uongozi ili viongozi wa kikabila waridhike.

Hawa wanafikiria kuwa mamlaka ambayo hupatikana kutoka kwa Wakenya unaweza kutumika na viongozi kuendesha wanachotaka,” aliongeza DP.

Alionekana kumshtumu Rais Uhuru akisema ni lazima kila kiongozi aheshimu katiba ya nchi hata kama sheria haimruhusu kupata anachotaka.

“Kama unachotaka ni kinyume na katiba, wewe ndio unafaa kubadili na wala si katiba kubadilishwa,” alisema Ruto.

Kambi za kisiasa za Rais na Raila zimekuwa zikipanga mabadiliko ya katiba kupitia mswada wa BBI.

Rais alisema mabadiliko yanayoletwa na refarenda ya BBI yananuwia kumaliza uhasama ambao umekuwa ukishuhudiwa kila mwaka wa uchaguzi nchini.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke