Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DP Ruto awasuta wakereketwa wa BBI asema wanashinikiza ajenda ya kibinafsi

1584ea7a1e139177 DP Ruto awasuta wakereketwa wa BBI asema wanashinikiza ajenda ya kibinafsi

Fri, 11 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Katika kile kilionekana kama kumrushia vijembe Rais Uhuru na Raila Odinga, Ruto alisema wengi wanashinikiza kuandaliwa rifarenda kwa faida zao wenyeweNaibu Rais alisema kila ajenda inatakiwa kuafikiana na katiba na kuwasaidia WakenyaMatamshi yake yanakujia mwezi mmoja baada ya Mahakama Kuu kuharamisha BBI

Naibu Rais William Ruto amewasuta wakereketwa wa Mpango wa Maridhiano (BBI) kwa kile alisema wanashinikiza rifarenda kwa faida zao za kibinafsi.

Ruto alikuwa miongoni mwa viongozi ambao walisherehekea uamuzi wa jopo la majaji watano ambao walifuta BBI ambao ni mradi uliozaliwa kutoka kwa handisheki ya Rais Uhuru Kenyatta na Raila Odinga.

Akizungumza baada ya kukutana na viongozi wa kidini katika makazi yake ya Karen Alhamisi, Juni 10, Ruto alisema kila ajenda inatakiwa kuafikiana na katiba na kuwasaidia Wakenya

"Endapo mahitaji ya walio mamlakani inaenda kinyume na katiba, si hatua ya katiba kubadilishwa lakini kile wanashinikiza ndio yatakiwa kuibadilisha," alisema.

Wiki chache zilizopita, Ruto pia alishambulia serikali anayohudumu akisema matatizo ya Kenya ni kutokana na uongozi mbaya na wala si katiba.

Ruto aliwahimiza viongozi kuzingatia masuala yanayowathiri Wakenya badala ya kushughulikia mambo ya kuwagawanya.

"Ningependa kuwaomba viongozi wa taifa letu kuwa kuna masuala kuu nchini kwa hivyo sisi sote tukuje pamoja tujadiliane si kuwa wabinafsi," alisema.

Matamshi yake yanakujia mwezi mmoja baada ya Mahakama Kuu kuharamisha BBI.

Kama TUKO.co.ke ilivyoripotia awali, Ruto kupitia kurasa zake za mtandao jamii alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa uamuzi huo ambao ulizima reggae ya BBI.

Hata hivyo, furaha ya Naibu Rais haikupokelewa vyema na wabunge wa Kieleweke ambao walimkashifu kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kuunga mkono miradi ya rais.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke